Home Makala Ajibu Atua Coastal Union

Ajibu Atua Coastal Union

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Coastal Union imetangaza kukamilisha usajili wa Ibrahim Ajibu ambaye alikua ni mchezaji huru baada ya kutemwa na klabu ya Singida Fountain Gate alipojiunga akitokea katika klabu ya Azam Fc.

Ajibu ambaye anatambulika kwa kipaji chake hasa akiwa katika klabu ya Yanga sc ambayo aliichezea kwa msimu mmoja na kisha kujiunga na Simba sc sehemu ambayo hakufanikiwa kupata namba kikosi cha kwanza.

Mchezaji huyo tayari ameshajiunga na timu hiyo katika kambi ya mazoezi iliyoko eneo la usagara na tayari ameshatambulishwa rasmi na mitandao ya kijamii ya klabu hiyo.

banner

Usajili wa kiungo huyo mshambuliaji umekuja kutokana na pendekezo la kocha Mwinyi Zahera ambaye alimfundisha akiwa katika klabu ya Yanga sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited