Home Soka Azam Fc Kukipiga na Wydad

Azam Fc Kukipiga na Wydad

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc usiku wa leo itaingia uwanjani katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Wydad Casablanca ya nchini Morocco mchezo utakaofanyika katika mji wa Benslimane nchini humo ikiwa ni mchezo wa kwanza mgumu kwa Azam Fc.

Azam Fc ambao juzi kulazimishwa sare ya 1-1 na Union Touarga,watakua na kazi ngumu ya kukabiliana na Wydad ya Rulani Mokwena ambaye alikua kocha wa Mamelod Sundowns ya nchini Afrika ya kusini kabla ya kutimuliwa kutokana na matokeo mabaya ya mabingwa hao.

Wydad ambao ni  mabingwa wa zamani wa Morocco na Afrika wanauchukulia mchezo huo kama kipimo kizuri cha mastaa wake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu ya nchini humo sambamba na michuano ya kimataifa.

banner

Azam Fc baada ya mchezo huo watakwenda jijini Kigali kucheza na Rayon Sports katika siku ya Rayon Day kisha watarejea nchini kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya kwanza ya ngao ya jamii dhidi ya Coastal Union siku ya Augusti nane katika uwanja wa Amani Visiwani Zanzibar.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited