Klabu ya Azam Fc imezindua rasmi jezi zake za msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya kimataifa mapema hii leo katika boti ya Azam Marine wakielekea Visiwani Zanzibar huku wakishuhudiwa na maelfu ya mashabiki kupitia Azam Tv.

Jezi hizo za aina tatu za nyumbani,Ugenini na jezi ya tatu zimezinduliwa mchana wa leo zikiwa na rangi nyeupe,Blue na Nyeusi huku zote zikiwa zimechanganywa na rangi ya dhahabu mbele ya Mh.Tabia Mwita ambaye ni Waziri wa michezo Visiwani Zanzibar.
Mpaka sasa tayari jezi hizo zinapatikana katika maduka mbalimbali Zanzibar na ndani ya jiji la Dar es salaam.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Msimu huu Azam Fc sambamba na kumaliza wa pili katika ligi kuu nchini pia watashiriki michuano ya kimataifa baada ya kupata nafasi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika na wanatarajiwa kuanza na Apr ya Rwanda katika hatua ya awali.
