Home Soka Azam Fc Yailaza Apr 1-0

Azam Fc Yailaza Apr 1-0

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imeanza michuano ya kombe la Klabu bingwa barani Afrika kwa ushindi kiduchu wa 1-0 dhidi ya Apr ya Rwanda katika mchezo wa hatua ya awali ya michuano hiyo uliofanyika katika uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam.

Ikianza na kikosi chake kinachoonekana ndio cha kwanza kikiwa na mastaa kama Mohammed Mustapha,Paschal Msindo,Lusajo Mwaikenda huku Yanick Bangala na Yeison Fuentes wakiwa kama mabeki wa kati na kiungo kikiongozwa na Adolph Mtasingwa Bitegeko na James Akaminko waliosaidia na Frank Tiesse na Gibril Sillah huku washambuliaji wakiwa ni Feisal Salum na Jhonier Blanco.

Azam Fc sambamba na kuwa na kikosi hicho bado walishindwa kupata bao lolote katika dakika 45 za kupindi cha kwanza huku wakipaswa kumshukuru kipa Mohammed Mustapha kwa kuokoa hatari kadhaa kutokana na mashambulizi ya kushtukiza kutoka kwa Apr.

banner

Feisal Salum alifanyiwa madhambi dakika ya 56 na mwamuzi kuamuru penati iliyopigwa kiufundi na Jhonier Blanco dakika ya 56 na kuipatia Azam Fc bao pekee katika mchezo huo.

Dakika tisini za mchezo huo zilitamatika kwa ushindi huo huku kibarua kikihamia jijini Kigali ambapo utapigwa mchezo wa marudiano wikiendi ya August 25 ambapo mshindi atavaana na mshindi baina ya Pyramid Fc dhidi ya Kvz ya visiwani Zanzibar.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited