Home Makala Azam Fc Yaipumilia Simba sc

Azam Fc Yaipumilia Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Ushindi wa mabao 2-1 ilioupata klabu ya Azam Fc dhidi ya Singida Black Stars umeisogeza timu hiyo mpaka nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini ikizidiwa na Simba sc kwa alama moja pekee.

Azam Fc baada ya kushinda mchezo huo imefikisha alama 27 huku Simba sc ikiwa na alama 28 huku Azam Fc ikiwa imecheza michezo 12 na Simba sc ikiwa na michezo 11.

Mabao ya Feisal Salum dakika ya 38 na lile la mshambuliaji raia wa Colombia Jhonier Blanco dakika ya 57 huku Elvis Rupia akifunga bao la kufutia machozi kwa Black Stars dakika ya 62 japo halikuzuia Azam Fc chini ya kocha Rachid Taoussi kuondoka na alama tatu muhimu katika mchezo huo.

banner

Idd Selemani “Nado” aliufanya mchezo huo kuwa mikononi mwake akitoa pasi zote mbili za mabao kwa pasi maridadi hali iliyompa tuzo ya uchezaji bora wa mchezo huo.

Singida Black Stars pamoja na kumsimamisha kocha Patrick Aussems na Dennis Kitambi bado imeendelea kutopata ushindi katika mchezo wa nne mfululizo katika ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited