Home Soka Azam Fc Yamtambulisha Staa wa Mali

Azam Fc Yamtambulisha Staa wa Mali

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imemtambulisha winga mshambuliaji Cheickna Diakite, akitokea katika klabu ya  soka ya Real Bamako inayoshiriki ligi kuu nchini Mali ambapo amesaini mkataba wa miaka mitatu kukaa Chamazi Complex mpaka mwaka 2027.

Diakite ni mshambuliaji anayetokea pembeni akisifika zaidi kwa kasi na chenga za maudhi huku akiwa na nguvu za kutosha kuisumbua ngome ya timu pinzani kwa dakika zote 90 za mchezo hasa ikichagizwa na umri wake wa miaka 19.

banner

Azam Fc iliwapasa kufanya kazi ya ziada kumnasa staa huyo ambaye alikua na ofa kutoka klabu kadhaa za kaskazini mwa Afrika ambazo zina nguvu kubwa kiuchumi sambamba na baadhi ya klabu barani ulaya hasa Ufaransa ambazo nazo zilivutiwa na uwezo wa staa huyo.

Mshambuliaji huyo amesajili kuchukua nafasi ya Kipre Jr ambaye ameuzwa kwa zaidi ya dola za kimarekana laki mbili kwenda katika klabu ya Usm Algers ya nchini Algeria na kuwafanya mabosi wa klabu hiyo kutafuta mbadala wake haraka ili isilete athari kwenye timu baada ya msimu uliopita Kipre Jr kufunga mabao 9 na kusaidia upatikanaji wa mabao 9 katika ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited