Home Soka Azam Fc Yawasili Rwanda

Azam Fc Yawasili Rwanda

by Sports Leo
0 comments

Msafara wa kikosi cha timu ya Azam fc umewasili salama nchini Rwanda kwa ajili ya mchezo wa pili wa  hatua za awali za michuano ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya APR Fc ya nchini humo.

Kikosi cha Azam Fc kimewasili nchini humo siku ya alhamis na mapema leo ijumaa kimeanza mazoezi kuikabili klabu hiyo inayomilikiwa na jeshi la nchi hiyo.

Azam Fc itakua na kibarua kikubwa cha kulinda ushindi wa 1-0 ilioupata dhidi ya timu katika mchezo wa kwanza uliofanyika katika uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es Salaam.

banner

Katika mchezo wa kwanza Azam Fc ilipata bao hilo kwa penati iliyopigwa na Jhonier Blanco baada ya Feisal Salum kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari.

Azam Fc inapaswa kupata sare ya aina yeyote ile ama isifungwe bao lolote ili kujiweka katika uhakika wa kufuzu hatua inayofuatia.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited