Home Makala Aziz Ki,Nouma Watemwa B/Faso

Aziz Ki,Nouma Watemwa B/Faso

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Yanga SC Stephane Aziz Ki na mlinzi wa Simba SC na Valentino Nouma wameachwa katika kikosi cha Burkina Faso kilichoitwa jana na kocha Brama Traore kwaajili ya michezo miwili ya kuwania kufuzu kombe la Dunia 2026

Burkina Faso itakuwa nyumbani Machi 16 2025 kucheza mchezo wake wa 5 wa hatua ya makundi dhidi ya Djibouti kabla ya kusafiri kuwafuata Guinea Bissau tarehe 23 Machi 2025

banner

Ikumbukwe kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 alikuwepo katika kikosi kilichocheza mechi za mwanzoni za michuano hiyo akicheza michezo mitatu na kutoa pasi moja ya goli

The Stallions wanashika nafasi ya 3 katika kundi A ikivuna alama 5 katika michezo minne iliyocheza, nyuma ya Guinea Bissau yenye alama 6 na Misri mwenye alama 10 anayeongoza msimamo wa kundi hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited