Home Makala Baleke Kutua Afrika Kusini

Baleke Kutua Afrika Kusini

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Amazulu imeanza mazungumzo na TP Mazembe ili kuinasa saini ya mshambuliaji,Jean Baleke ambaye alikuwa akiitumikia klabu ya Yanga sc kwa mkopo wa mwaka mzima kabla ya mkataba huo kusitishwa.

Amazulu wamehamia kwa Baleke baada ya kuikosa saini ya Frank Ssebufu raia wa Uganda ambaye alikuwa akiitumikia New York Redbull II ya MLS.

Inaelezwa kuwa TP Mazembe wanahitaji angalau Dolan 80,000 ili kumuachia jumla Jean Baleke ambaye aliwahi kuitumikia klabu ya Simba Sc kwa misimu takribani miwili.

banner

Baleke ameachwa na Yanga sc baada ya kocha Sead Ramovic kutoridhishwa na uwezo wake kutokana na kuonyesha kiwango cha kawaida uwanjani ambapo alifanikiwa kucheza michezo miwili pekee ya ligi kuu chini ya kocha aliyetimuliwa Miguel Gamondi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited