Home Makala Banda Kuvuna Mamilioni Richard Bay

Banda Kuvuna Mamilioni Richard Bay

by Sports Leo
0 comments

Beki Mtanzania Abdi Banda anajiandaa kupokea Mamilioni kutoka katika Klabu ya Richard Bay inayoshiriki ligi kuu nchini Afrika ya kusini baada ya kushinda kesi yake dhidi ya klabu hiyo.

Banda alifungua kesi katika Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kupitia combo chake maalumu cha kusimamia malalamiko ya mikataba kwa wachezaji ambapo iliamuriwa klabu hiyo imlipe Staa huyo kiasi cha shilingi milioni 360 za kitanzania.

Fifa katika kukazia hukumu hiyo imeifungua klabu hiyo kufanya usajili wa wachezaji wapya mpaka pale itakapomlipa staa huyo ambaye kwa sasa anaichezea Dodoma Jiji Fc kwa mkataba wa miezi sita.

banner

Hii si mara ya kwanza kwa Banda kulipwa Mamilioni ambapo msimu uliopita alilipwa takribani kiasi cha shilingi milioni 180 baada ya klabu ya Chipa United kuvunja mkataba na staa huyo.

Banda tangu aachane na Simba sc amekua hatulii katika timu nyingi hasa za nje ya nchi ambapo alizichezea klabu za Baroka Fc,Chipa United,Mtibwa Sugar na Dodoma Jiji.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited