Home Soka Bodi ya Ligi Yamshukia Gamondi

Bodi ya Ligi Yamshukia Gamondi

by Sports Leo
0 comments

Kamati maalumu ya usimamizi wa ligi kuu chini ya bodi ya ligi kuu nchini imempiga faini ya shilingi milioni mbili aliyekua kocha wa klabu ya Yanga sc Miguel Gamondi kwa kosa la kumsukuma kocha msaidizi wa klabu ya Singida Black Stars Sliman Marloen katika mchezo wa ligi kuu namba 32 uliofanyika katika uwanja wa New Amaan complex Visiwani Zanzibar.

Katika mchezo uliokua na presha kwa pande zote ambapo Yanga sc ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa 1-0 lililofungwa na Pacome Zouzoua ambapo kulikua na kurushiana maneno baina ya mabenchi ya ufundi wa timu hizo na ndipo Gamondi alipofanya kosa hilo.

Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 45:2(2:1) ya ligi kuu nchini ambapo sambamba na kupigwa faini hiyo pia ataikosa michezo mitatu ya ligi kuu nchini ama michuano ya kombe la Shirikisho la Crdb.

banner

Hata hivyo Gamondi tayari ameshatimuliwa klabuni hapo hivyo kuna adhabu atazikwepa kwa sasa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited