Home Soka C.E.O Namungo Akimbia Vipigo

C.E.O Namungo Akimbia Vipigo

by Sports Leo
0 comments

Afisa mtendaji mkuu wa klabu ya Namungo Fc Omary Kaya ameamua kujiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na vipigo mfululizo ambavyo timu hiyo imevipata msimu huu.

Kaya ameandika barua ya kuachia ngazi baada ya timu yake kuruhusu kipigo cha mabao 2-0 kutoka Fountain Gate Fc siku ya Alhamis August 29 huku pia ikifungwa 2-1 na Tabora United katika uwanja wa nyumbani wa Majaliwa.

“Mimi Omary Kaya siku ya leo tarehe 30 August 2024 nimewasilisha kwa Uongozi barua ya kujiuzuru nafasi ya utendaji mkuu wa Klabu Namungo Fc”Ilisomeka taarifa hiyo huku ikiendelea kusema.

banner

“Hivyo napenda kuwashukuru Uongozi,benchi la ufundi,wachezaji na mashabiki wote wa klabu ya Namungo katika kipindi chote nilichotumikia klabu kwa Ushirikiano wao kama familia”.

Kutokana na taarifa hiyo tayari klabu hiyo imekubali taarifa hiyo na kuthibitisha kukubaliana na barua hiyo ya kujiuzuru.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited