Home Makala Caf Yairudisha Simba Sc Zanzibar

Caf Yairudisha Simba Sc Zanzibar

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Soka barani Afrika (Caf) limeamuru mchezo wa fainali ya pili ya kombe la Shirikisho barani Afrika baina ya klabu ya Simba Sc dhidi ya Rs Berkane kuchezwa katika uwanja wa Amaani Complex Visiwani Zanzibar badala ya Benjamin Mkapa kama ilivyotarajiwa.

Mchezo huo uliopangwa kuchezwa hapa nchini Mei 25 2025 awali ilitarajiwa utafanyika jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Benjamin Mkapa lakini baada ya wakaguzi kutoka Caf kuukagua uwanja huo mara kwa mara wamejiridhisha kwamba haufai.

Sababu kubwa kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wakaguzi hao ni kwamba sehemu ya kuchezea ya uwanja huo inahifadhi maji kipindi hichi cha mvua na hivyo mpira hautachezwa kwa utulivu mkubwa.

banner

Mpaka sasa klabu ya Simba Sc na Serikali kupitia Shirikisho la Soka nchini (TFF) wameshapewa taarifa hiyo na wanajaribu kupambana kuona kama wanaweza kuwashawishi Caf kubadili uamuzi huo.

Endapo Caf itaendelea kushikilia msimamo huo maana yake ni kwamba Berkane watakua wamepata nafuu kutokana na uwanja wa Amaani Complex kuchukua idadi ndogo ya mashabiki tofauti na Benjamin Mkapa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited