Mshambuliaji wa AzamFc ,Obrey Chirwa ameipeleka klabu yake ya zamani Yanga katika shirikisho la soka duniani (FIFA) kutokana na madai ya fedha ambayo anaidai timu hiyo kwa kipindi cha miaka miwili aliyoitumikia.
Baada ya mchezaji huyo kuondoka na kwenda kuitumikia timu ya Nogoom Fc ya Misri alijaribu kuwatumia barua uongozi wa timu hiyo na kuwaomba pesa zake ambazo alitakiwa kupata baada ya kusaini mkataba.
\Ukimya ulitawala na baadaye Chirwa aliamua kufuata kanuni na kwenda TFF kuwaelez akiwa na barua niliyoitumia Yanga isiyokuwa na majibu yoyotte tangu mwaka upite.
“FIFA wamenipatia barua ambayo nitapeleka ofisi za Yanga zilizopo Jangwani na baada ya muda mfupi nategemea kupata majibu kutoka FIFA,lllini na kwa njia gani nitapata pesa zangu kwani wao wana jukumu la kusimamia hili kwa hapa lilipofikia”alisema Chirwa