Baada ya kuachana na Kipa wake Raia wa Congo Dr Ley Matampi sasa klabu hiyo imetangaza kuachana na beki wake Hernest Malonga pamoja na Deus Lucas baada ya kuvunja mkataba wake klabuni hapo.
Malonga mchezaji wa zamani wa klabu ya Ihefu Fc ambayo sasa ni Singida Black Stars anaondoka klabuni hapo kwa makubaliano na uongozi wa Klabu hiyo kuvunja mkataba huo.
Pia uongozi wa klabu hiyo chini ya kocha Juma Mwambusi umeendelea na kusafisha kikosi hicho ili kuruhusu kufanya sajili mpya zenye tija kikosini humo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini Coastal Union ina alama 16 katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ikiwa imecheza michezo 13 tu.

