Home Soka Coastal Union Yashusha Straika Mmali

Coastal Union Yashusha Straika Mmali

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Coastal Union ya Jijini Tanga imesajili mshambuliaji Amara Bagayoko raia wa Mali ili kuongeza ufanisi katika safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 amesajiliwa akitokea katika ligi kuu ya Togo ambapo alikua amefunga jumla ya mabao 19 katika ligi hiyo.

Usajili huo umepitishwa na kocha Juma Mwambusi ambapo umelenga kuongeza ufanisi wa ufungaji ambapo katika michezo 15 ya ligi kuu ya Nbc nchini klabu hiyo imefunga mabao 15 pekee.

banner

Staa huyo baada ya kusaini mkataba mfupi mpaka mwisho wa msimu huu tayari ameshawasili jijini Arusha ilipo kambi ya klabu hiyo tayari kwa michezo ijayo ya ligi kuu ya Nbc nchini.

Katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini klabu hiyo imecheza michezo 15 ikiwa katika nafasi ya 10 ikiwa na alama 17 pekee.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited