Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba sc Hassan Dilunga yupo mbioni kufanyiwa upasuaji wa goti baada ya kuumia na huenda akakosa michezo yote ya klabu ya Simba sc iliyobakia msimu huu.
Dilunga mwenye uwezo wa kucheza nafasi zote za kiungo amekosekana uwanjani kwa muda mrefu kutokana na majeraha hayo na tayari uongozi wa klabu ya Simba sc unampango wa kumfanyia upasuaji.