Home Makala Fainali Cafcc Kumalizikia B/Mkapa

Fainali Cafcc Kumalizikia B/Mkapa

by Sports Leo
0 comments

Imefahamika kuwa klabu ya Simba Sc itacheza mchezo wake wa marudiano wa Fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Rs Berkane katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Fainali hizo zitachezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itachezwa nchini Morocco Mei 17 2025 na marudiano kufanyika nchini Mei 25 2025.

banner

Simba sc imefanikiwa kufuzu fainali hizo baada ya kuifunga Stelleboch Fc kwa matokeo ya jumla ya 1-0 baada ya kutoka suluhu katika mchezo wa marudiano nchini Afrika ya kusini huku mchezo wa kwanza Visiwani Zanzibar Simba sc iliibuka na ushindi wa 1-0.

Mchezo wa pili wa fainali huwa na faida kwa klabu mwenyeji kutokana na mchezo huo kuwa ndio maalumu wa kukabidhi kombe na huwa na msisimko mkubwa wa mashabiki wa nyumbani.

Simba sc inapewa nafasi kubwa ya kutwaa kombe hilo ambalo halijawahi kuchukuliwa na klabu yeyote hapa nchini Tanzania.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited