Home Makala Hapatoshi Ufaransa Vs Morocco Nusu Fainali Wc

Hapatoshi Ufaransa Vs Morocco Nusu Fainali Wc

by Sports Leo
0 comments

Patachimbika ndio neno linalofaa kulitumia kuelekea mchezo wa nusu fainali katika ya Ufaransa na Morocco katika michuano ya kombe la dunia linaloendelea nchini Qatar ambapo wadau wa soka duniani wamekua wakiusubiri kwa hamu mchezo huo.

Morocco imefuzu hatua ya nusu fainali baada ya kuifunga Ureno 1-0 huku Ufaransa ikiifunga Uingereza 2-1 katika michezo ya robo fainali iliyochezwa wikiendi iliyopita.

Ufaransa atakua na kazi ya ziada kuifungua safu ya ulinzi ya Morocco ambayo imefanikiwa kutoruhusu magoli katika michezo dhidi ya Hispania na Ureno na kuwa timu ya kwanza barani Afrika kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo mikubwa duniani.

banner

Mashabiki wengi wa nchi za kiarabu na Afrika watagawanyika katika kushabikia timu hizo kwa sababu Ufaransa ina raia wengi kutoka nchi za Afrika Magharibi ikiwemo Morocco,Algeria pamoja na nchi za kiafrika zinazozungumza kifaransa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited