Home Soka Hispania Yatwaa Euro 2024

Hispania Yatwaa Euro 2024

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Hispania imefanikiwa kuchukua taji la michuano ya Euro 2024 iliyokua ikifanyika nchini Ujerumani baada ya kufanikiwa kuifunga England kwa mabao 2-1 katika fainali ya michuano hiyo iliyofanyika katika uwanja wa Olympia jijini Berlin,Ujerumani.

Hispania ambayo haijapoteza hata mchezo mmoja katika michuano hiyo ilionyesha dalili za kutwaa ubingwa huo mapema kuanzia mwanzo wa mchezo baada ya kuumilika mchezo kwa kiasi kikubwa huku Nico Williams akiwatanguliza na bao la mapema dakika ya 47 ya kipindi cha pili akimalizia pasi safi ya Lamine Yamal.

Bao hilo lilisawazishwa na Cole Palmer dakika ya 73 ikiwa ni muda mchache baada ya kuingia uwanjani lakini furaha haikudumu kwani zikisalia dakika nne mchezo kumalizika Mikel Oyalzabal alifunga bao la pili akipokea pasi safi ya Cucurella.

banner

Mwamuzi wa kati baada ya dakika nne za nyongeza alimaliza mchezo na kuzua shangwe kwa Wahispania waliojaa uwanjani hapo ambapo pamoja na kombe pia mchezaji Rodri alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa michuano hiyo huku kinda Yamal akitwaa tuzo ya mchezaji bora kijana.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited