Inadaiwa kwamba Manchester United wako tayari kubadilishana Paul Pogba na James Rodriguez pamoja na kiasi cha fedha huku wakala Jorge Mendez akihusishwa kufanikisha dili hilo.
United wako tayari kumuachia Pogba kwa dau la paundi milionin 150 huku kushamili kwa ugonjwa wa Corona kumesababisha ligi mbalimbali kusimamishwa hivyo klabu nyingi kuyumba kimapato hivyo dirisha la usajili kutokua na ushindani hali inayopelekea ugumu kumuuza Pogba kwa bei iliyopangwa na United hivyo mabadalishano yanaweza kuwa uamuzi mzuri zaidi.
Licha ya Man United pia klabu za Everton inayonolewa na Carlo Ancelot mkufunzi wa zamani wa klabu ya Real Madrid pamoja na Tottenham zinamhitaji kiungo huyo.