Home Soka Kaizer Chief Yamtaka Maxi Nzengeli

Kaizer Chief Yamtaka Maxi Nzengeli

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Kaizer Chiefs Fc imeonyesha kuvutiwa na mchezaji Maxi Nzengeli ambapo mabosi wa klabu hiyo wameanza mazungumzo na mabosi wa Yanga sc kumhitaji nyota huyo mzaliwa wa Kindu nchini Dr Congo ambaye Yanga sc ilimsajili msimu uliopita.

Nyota huyo licha ya kwamba ana mkataba wa mwaka mmoja na Yanga sc tayari mabosi wa klabu hiyo wameanza mchakato wa kumuongezea mkataba na wameshafungua mazungumzo na wakala wa mchezaji huyo juu ya dili hilo jipya.

Mpaka sasa msimamo wa mabosi wa Yanga sc ni kutomuacha staa huyo asajiliwe na timu nyingine ambapo wana malengo makubwa msimu huu ya kutwaa taji la ubingwa wa Afrika baada ya kunogewa msimu uliopita ambapo ilibaki kidogo wafuzu hatua hiyo kama sio makosa ya mwamuzi wa video kukataa bao la Aziz Ki.

banner

Msimu huu pamoja na Yanga sc kuwaongeza mastaa wakubwa eneo la kiungo cha ushambuliaji lakini bado nafasi ya Nzengeli inaonekana kutokana na umuhimu wake kikosini hasa uwezo wake wa kushambulia na kukaba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited