Bondia Twaha Kiduku anatarajiwa kupanda ulingoni siku ya Jumamosi kuzichapa na Alex Kabangu katika pambano la uzito wa kati la kuwania ubingwa wa UBo litakalofanyika mkoani morogoro.
Pambano hilo la raundi nane litafanyika mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwa kina Kiduku ambapo viingilio vitakua ni elfu 10 na ishirini huku upande wa viti maalumu itakua elfu 30.
Mratibu wa pambano hilo, Bakari Khatibu amesema kuwa maandalizi ya pambano yamekamilika kwa asilimia 100 huku akiwataka wadau wangumi nchini kujitokeza kwa wingi kushuhudia pambano hilo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Maandalizi kwa upande wetu ni mazuri tunashukuru Mungu tayari Kabangu ameshaingia na yupo hapa Morogoro, tunachosubiria ni siku kufika kwa ajili ya mambo mengine”.

