Bosi wa klabu ya Simba sc Mohamed Dewji ameamua kuwakabidhi faili zima la usajili wa mastaa klabuni hapo kwa gwiji Crescentius Magori pamoja na Mulamu Ng’ambi ili kurejesha furaha kwa mashabiki wa klabu hiyo kutokana na klabu hiyo kutofanya vizuri kwa mwaka wa tatu sasa.
Sababu kubwa ya kufanya ni baada ya kuona kuwa pesa za usajili zinatoka lakini mastaa wanaosajiliwa klabuni hapo hawana viwango vya kuitumikia klabu hiyo hivyo bora kuwarejesha wakongwe hao ambao waliipa Simba sc nyakati za furaha kwa takribani miaka minne mfululizo.
Wawili wataungana na Babrah Gonzalez ambaye anaweza kurejeshwa kama Mtendaji mkuu wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Iman Kajula ambaye ataondolewa mwishoni mwa msimu huu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Magori ndie aliwasajili mastaa kama Rally Bwallya,Gerson Fraga,Luis Miqquisone,Erasto Nyoni,Aishi Manula na Shomari Kapombe,Pascal Wawa na wengineo ambao waliifanya klabu ya Simba sc itambe kwa miaka minne mfululizo nchini huku ikifika hatua ya robo fainali katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika.
