Home Soka Manula Atemwa Simba Sc Ikiifuata Bravos

Manula Atemwa Simba Sc Ikiifuata Bravos

by Sports Leo
0 comments

Kipa Aishi Manula ametemwa katika msafara wa kikosi cha timu ya Simba sc kilichoondoka mapema leo kuelekea nchini Angola kuivaa klabu ya Bravos do Marquiz ya nchini humo katika mchezo wa marudiano wa hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Katika msafara huo wa wachezaji 22 jina la Manula halimo huku mpaka sasa hakuna sababu iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo ambapo makipa Moussa Camara,Ally Salim na Hussein Abel ndio wameondoka na kikosi.

banner

Maisha ya Manula katika klabu ya Simba Sc yamekua na wakati mgumu tangu aliporuhusu bap 5-1 kutoka kwa Yanga sc katika mchezo wa ligi kuu mwanzoni mwa mwaka jana.

Simba sc itawavaa Bravos katika mchezo muhimu ambao inapaswa kushinda ili kufuzu moja kwa moja hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited