Home Makala Mgunda Ashindwe Mwenyewe

Mgunda Ashindwe Mwenyewe

by Sports Leo
0 comments

Mabosi wa klabu ya Simba sc wamempa kocha Juma Mgunda huduma sawa na wanazopewa makocha wa kigeni wakiwemo kina Zoran Maki na Didier Gomez walipokua wakiifundisha klabu hiyo kwa nyakati tofautitofauti baada ya kumpatia nyumba na gari ya kutembelea pamoja na dereva.

Nyumba hiyo aliyopewa Mgunda ina hadhi kubwa na ipo karibu na bahari huku pia akipewa gari kali aina ya Tata ambayo ataitumia mazoezi na katika misafara rasmi ya klabu hiyo ili kumpa hadhi sawa na makocha wa kigeni na kumtuliza akili ili aifanye kazi yake ipasavyo.

Mabosi wa klabu ya Simba sc wameamua kufanya hivyo ili kumpa morali pamoja na kuhakikisha anafanya maamdalizi mazuri kuelekea mchezo dhidi ya Premero De Augosti ya Angola na michezo ya ligi kuu nchini huku wakitaka kuhakikisha mpaka januari wawe wamepata kocha mpya ambaye atakuta timu imeandaliwa vyema na Mgunda.

banner

Kocha huyo amejiunga na Simba sc kama kocha wa muda akitokea klabu ya Coastal Union kuja kuchukua nafasi ya kocha Zoran Maki ambaye alikubalina na uongozi wa klabu hiyo kuvunja mkataba kwa maslhai ya pande zote mbili na kwenda kujiunga na klabu ya All Ittihad ya nchini Misri.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited