Tajiri wa klabu ya Simba sc ameongeza nguvu katika usajili wa beki wa Cotton Sports ya nchini Cameroon Che Fondoh Malone ili atue msimbazi kusaidiana na Henock Inonga katika eneo la ulinzi la klabu hiyo.
Awali Simba sc walipeleka ofa ya dau la usajili la dola elfu arobaini ambalo limekataliwa na klabu hiyo wakidai halitoshi wakitaka walipwe kiasi cha dola laki na hamsini ili wamuachie beki huyo mwenye akili ya mpira na mwili wa mazoezi.
Sasa tayari Simba sc imewasilisha ofa ya pili ambayo ni dola elfu sabini ikiwa takribani ni nusu ya dau wanalohitaji klabu yake huku inasemekana kuwa tajari wa klabu hiyo Mohamed Dewji amewataka kuhakisha kuwa beki huyo anasajili haraka kutokana na klabu hiyo kuwa na bajeti ya usajili tayari.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Simba sc inapambana kukamilisha usajili wa beki huyo ili wamuache Joash Onyango ambaye ameomba kuondoka klabuni hapo mara kadhaa.