Home Makala Morrison Kuikosa Simba sc

Morrison Kuikosa Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Benard Morrison amefungiwa mechi tatu mfululizo na kamati ya usimamizi wa ligi kuu nchini kwa kosa la kumkanyaga mchezaji Lusajo Mwaikenda katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc uliomalizika kwa sare ya 2-2.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka bodi ya ligi kuu nchini adhabu hiyo imetolewa na bodi ya ligi kuu nchini kwa uzingativu wa kanuni ya 42:5(5.6) ya ligi kuu kuhusu udhibiti wa wachezaji.

Morrison kutokana na adhabu hiyo ataikosa michezo mitatu dhidi ya Namungo Fc,Ruvu Shooting Fc na dhidi ya mahasimu wao wakubwa Simba sc mchezo ambao mashabiki wa klabu ya Yanga sc wangependa ashiriki ili kuwalipiza kisasi watani hao wa jadi.

banner

Hii si mara ya kwanza kwa Morrison kufungiwa kwani imekua ni kawaida kwake kutokana na kuwa na utovu wa nidhamu huku pia akikabiliwa na matukio tata kiwanjani mara nyingi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited