Klabu ya Simba Sc iko mbioni kukamilisha usajili wa mchezaji Ellie Mpanzu kutoka klabu ya As Vita ya nchini Congo Dr baada ya kufikia makubaliano ya maslahi binafsi na mchezaji huyo ambaye muda wowote anaweza kutua hapa nchini kwa ajili ya kukamilisha taratibu za mwisho za usajili.
Mpanzu mwenye miaka 22 yupo katika orodha ya wachezaji wanaowindwa na Simba sc tangu mwanzoni mwa msimu huu wakati wa usajili wa dirisha kubwa lakini dili hilo halikufanikiwa na badala yake akasajiliwa Willy Esomba Onana ambaye ameshindwa kukidhi matarajio.
Mpanzu amemaliza msimu akiwa na mabao 11 akicheza zaidi kama winga wa kulia ama kushoto huku pia akiwa na uwezo mzuri wa kucheza kama mshambuliaji namba mbili.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Msimu huu Simba sc imepanga kufanya maboresho makubwa ya kikosi chake kwa kusajili majembe ya maana huku ikilenga zaidi kusajili vijana ambao watadumu kikosini humo kwa miaka kadhaa ili kurejesha heshima yao iliyopotea baada ya kukosa makombe kwa msimu wa tatu mfululizo sasa.

