Home Makala Mpole Ajiunga na Kagera Sugar

Mpole Ajiunga na Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa zamani wa klabu ya Geita Gold na FC Lupopo ya Dr Congo George Aman Mpole amejiunga na klabu ya Kagera Sugar baada ya kuachana na klabu ya Pamba aliyoitumikia kwa nusu msimu pekee.

Mpole hakuwa na wakati mzuri kwenye kikosi cha Pamba tangu aliposajiliwa kwenye dirisha kubwa msimu huu kama mchezaji huru baada ya kuachana na FC Lupopo ya DR Congo.

Tayari klabu ya Kagera Sugar imemtambulisha mchezaji huyo ambaye anachukua nafasi ya Obrey Chirwa ambaye amejiunga na Kengold Fc ya jijini Mbeya.

banner

Mbali na Mpole klabu hiyo pia imekamilisha usajili wa kipa wa Klabu ya Simba Sc Ahmed Feruzi kwa mkopo wa nusu msimu sambamba na Shaphan Oyugi Siwa kutoka ligi ya Kenya.

Kagera sugar chini ya kocha Mellis Medo imeendelea na mazoezi makali kujiandaa na michezo ya ligi kuu nchini ambapo itaanza kucheza na Yanga sc mchezo wa kiporo mapema mwezi ujao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited