Home Makala Mtibwa Yafungiwa Kusajili Fifa

Mtibwa Yafungiwa Kusajili Fifa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Mtibwa Sugar imefungiwa kusajili na Shirikisho la soka Duniani (Fifa) kutokana na kutokamilisha malipo ya fedha za usajili za mchezaji Justin Ndikumana ambaye ilimsajili klabuni hapo msimu uliopita.

Fifa iliwataka Mtibwa Sugar kulipa kiasi kinachokadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni 34 za kitanzania ambapo walipewa siku 45 kukamilisha malipo hayo.

Sasa rasmi baada ya Mtibwa Sugar kushindwa kukamilisha malipo hayo sasa wamefungiwa rasmi kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Fifa na nakala yake kupatiwa wahusika.

banner

Mtibwa Sugar wamefungiwa kusajili wachezaji wa ndani pamoja na wale wa kigeni mpaka hapo watakapolipa kiasi hicho tajwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited