Home Soka Mvp wa Ivory Coast Atua Simba sc

Mvp wa Ivory Coast Atua Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imekamilisha usajili wa kiungo Mshambuliaji Ahoua Jean Charles kutokea klabu ya Stella Club Abijani ya nchini Ivory Coast kwa mkataba wa miaka miwili kuja kurejesha ufalme uliopotea Msimbazi kwa muda wa miaka mitatu sasa.

Kiungo huyo ndie mchezaji bora wa ligi kuu ya nchini Ivory Coast kwa msimu huu akifanikiwa kufunga mabao 12 na kutoa pasi za mabao 9 na kufanya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora kwa msimu huu ulioisha nchini humo huku pia akizikaa ofa nyingi za Afrika Magharibi ambapo timu kadhaa zilikua zinamtolea macho.

Kiungo huyo anakuja kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Cletous Chama ambaye amejiunga na Yanga sc kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza mwingine licha ya jitihada za makusudi za mabosi wa klabu hiyo kumuongezea mkataba wa kusalia klabuni hapo.

banner

Mpaka sasa Simba sc imewasijili Lameck Lawi,Stephen Mukwala na Joshua Mutale huku ikiwaongezea mikataba mastaa Kibu Dennis,Mzamiru Yassin na Israel Mwenda kuendelea kusalia klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited