Home Makala Ninja Kutua Geita Gold Sc

Ninja Kutua Geita Gold Sc

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Yanga sc Abdalah Shaibu ‘Ninja’ ameuomba uongozi wa klabu ya Yanga sc kumruhusu kwenda kwa mkopo katika klabu ya Geita Gold Sc ambayo imeonyesha nia ya kumsajili kwa mkopo wa msimu mzima.

Ninja ambaye amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Yanga sc baada ya kocha Nabi kumhitaji kikosini licha ya uongozi wa klabu hiyo kuonyesha nia ya kutomuongezea mkataba ambao ulikua umeisha na tayari alikua amesharejea nyumbani kwao Zanzibar kujipanga kutafuta timu nyingine.

Geita Gold Sc ambayo itashiriki michuano ya kimataifa ya Kombe la shirikisho ipo katika harakati za kujenga kikosi chake ili kupata uhakika wa kufanya vizuri zaidi katika michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi za vilabu barani Afrika.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited