Home Makala Onana Aondoka Simba Sc

Onana Aondoka Simba Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imetangaza kuachana na mshambuliaji Leandre Willy Esomba Onana baada ya kufikia makubaliano baina ya pande zote mbili kuachana kwa maslahi yao wote.

Onana aliyesajiliwa na Simba sc akitokea klabu ya Rayon Sports ya Rwanda ambapo aliibuka mfungaji bora msimu wa 2022/2023 na kuwavutia mabosi wa Simba Sc walioamua kuvunja benki kumsajili.

Msimu uliopita Onana hakua na msimu mzuri klabuni humo akishindwa kuwashawishi walimu Roberto Oliveira “Robertinho” na Abdelhack Benchika na kuishia kuwekwa benchi mara kwa mara.

banner

Msimu huu Mwalimu Fadlu Davis ameridhia kuondoka kwa Onana ambaye anakwenda kujiunga na klabu Al Ahly Benghazi ya nchini Libya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited