Home Makala Pablo Kusalia Simba sc

Pablo Kusalia Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klabu ya Simba sc umeamua kwa pamoja kusalia na kocha Pablo Franco pamoja na kutotimiza masharti aliyopewa kwenye mkataba wake ya kuhakikisha kuwa klabu hiyo inatwaa makombe yote na kufika hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la shirikisho ama klabu bingwa barani Afrika.

Kocha huyo raia wa Hispania amebahatika kusalia klabuni hapo baada ya kufanikiwa kuifikisha klabu hiyo hatua ya robo fainali ya kombe la shirikisho huku pia kitendo cha kutolewa kwa matuta na Orlando Pirates huku wakishinda mchezo wa kwanza jijini Dar es salaam kikimbeba kiasi cha kuwashawishi viongozi kumuongezea muda zaidi huku wakimpa mamlaka yote ya usajili wa mastaa wa kikosi hicho msimu ujao huku akichagua wachezaji wa kuwatema.

Pablo aliikuta Simba sc ikiwa imetolewa na Jwaneng Galaxy Fc katika kombe la klabu bingwa barani Afrika na kusababisha kocha Didier Gomez kutimuliwa klabuni hapo na kuletwa Pablo kuchukua nafasi yake ambapo alikuta tayari mastaa wakiwa wamesajiliwa tayari huku yeye akiwa na kazi ya kuwatengeneza.

banner

Inasemekana pamoja na kubakishwa klabuni hapo kocha huyo ana kazi ya kuhakikisha Simba sc inatwaa taji la tano mfululizo la ligi kuu mbele ya Yanga sc anayeongoza ligi akiwa na alama 53 huku Simba sc akiwa na alama 40 na mchezo mmoja mkononi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited