Rais Samia Aishukia Ccm Kuhusu Viwanja

by Dennis Msotwa
0 comments

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo amezungumzia suala la ubovu wa viwanja vya soka nchini huku akikitaka chama cha mapinduzi(Ccm) kukarabati viwanja ambavyo wanavimiliki ama wawakaribishe wawekezaji waviendeshe viwanja hivyo.

Rais huyo wa kwanza mwanamke nchini Alisema hayo wakati anahutubia vijana wa jiji la Mwanza katika mkutano maalumu ambapo ulitoa fursa kwa vijana kuongea na Rais huyo kuelezea changamoto mbalimbali katika mkutano uliofanyika katika uwanja wa Nyamagana katikakati ya jiji.

“Viwanja vingi vya Michezo vinamilikiwa na Chama cha Mapinduzi nakiomba chama kikarabati viwanja hivyo na Kama wanashindwa basi watafute wawekezaji ili viwanja viwekwe nyasi za bandia kwani michezo ni ajira”Alisema Rais Samia

You may also like

Leave a Comment

Enable Notifications OK No thanks