Home Makala Ramovic Asepa Yanga Sc

Ramovic Asepa Yanga Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imetangaza kuachana na kocha wake Sead Ramovic kwa makubaliano ya pande zote mbili baada ya kuafikiana kuvunja mkataba wa kocha huyo aliyedumu takribani miezi mitatu klabuni hapo.

Taarifa iliyotolewa na idara ya habari ya klabu hiyo imesema kuwa katika mchezo wa kesho wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Kengold Fc timu hiyo itakua chini ya kocha msaidizi Abdulhamid Moalin.

banner

Ramovic anaondoka pamoja na kocha msaidizi Mustafa Kodro ambapo taarifa za chini ya kapeti zinasema kuwa kocha huyo amepata ofa nono katika klabu ya Cr Belouzdad ya nchini Algeria.

Tayari klabu hiyo imetangaza kocha wa klabu ya Singida Black Stars Miloud Hamdi kuchukua nafasi ya Ramovic klabuni hapo.

Miloud ambaye amejiunga na Singida Black Stars lakini bado hajafanikiwa kukaa benchi hata mechi moja tangu ajiunge na timu hiyo ambapo ameishia kuinoa timu hiyo kambini jijini Arusha tu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited