Home Makala Rashford Atua Aston villa

Rashford Atua Aston villa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Aston Villa imethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Marcus Rashford raia wa England kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu huu 2024-2025 akitokea Manchester United.

Aston Villa italipa asilimia 75 ya mshahara wa Rashford hadi mwezi Juni mwaka huu huku kukiwa na kipengele cha kumnunua jumla kwa ada ya pauni milioni 40.

banner

Rashford (27) ambaye alijiunga na Mashetani hao Wekundu akiwa na umri wa miaka saba anaondoka klabuni hapo baada ya miaka 20 akiwa amepachika magoli 138 kwenye michezo 426.

“Nimefurahi sana kutua kwenye kikosi cha Aston Villa. Nilikuwa na bahati ya timu nyingi kunitaka, lakini Villa lilikuwa chaguo langu rahisi sana, napenda jinsi wanavyocheza msimu huu, nifuraha kuwa hapa na nasubiri kwa hamu kubwa siku ya kuingia uwanjani,” alisema Rashford wakati anatambulishwa.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa mshambuliaji huyo ambaye ameitumikia timu ya Taifa ya England mechi 60 anatarajiwa kuendelea kupokea kitita chake kilekile cha mshahara cha pauni 350,000 kwa wiki na mkataba wake na United unatarajiwa kumalizika Juni 2028.

 

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited