Home Soka Simba Sc Kurudi kwa Fei Toto

Simba Sc Kurudi kwa Fei Toto

by Sports Leo
0 comments

Kwa mujibu wa taarifa za ndani Klabu ya Simba Sc itatuma rasmi maombi ya kumuhitaji Kiungo wa klabu ya Azam Fc Feisal Salum ili kukiongezea nguvu kikosi hicho hasa katika michuano ya Kimataifa.

Simba Sports Club inamuhitaji kuanzia dirisha dogo lakini pia itakuwa tayari kusubiri hadi dirisha kubwa kama itashindikana kwenye dirisha la usajili la mwezi Januari.

Feisal amebakisha mkataba wa miaka miwili ya kusalia Azam Fc baada ya kumsajili kwa mkataba wa miaka mitatu msimu uliopita akitokea Yanga sc.

banner

Azam Fc na Yanga sc waliweka vipengele vya kuitaarifu Yanga sc endapo watakua na mpango wa kumuuza staa ndani ya nchi huku pia wakiweka dau la dola laki 5 kwa timu inayotaka kumnunua staa huyo.

Simba sc itakutana na upinzani mkubwa kutoka Yanga sc ambao nao wanamhitaji staa huyo arejee klabuni hapo ikiwa ni miaka mmoja tangu aondoke kwa usajili ambao ulileta mtafuruku kiasi cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk.Samia Suluhu Hassan kuingilia kati.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited