Home Makala Simba Sc Yaachana na Kennedy Juma

Simba Sc Yaachana na Kennedy Juma

by Sports Leo
0 comments

Ndoa baina ya beki Kennedy Juma na klabu ya Simba sc imefikia tamati rasmi hii leo baada ya klabu hiyo kutangaza kauchana na staa huyo mchana wa leo baada ya mkataba wake kufikia tamati.

Kennedy alisajiliwa na Simba sc mwaka 2019 akitokea timu ya Singida United ambapo sasa anaondoka kama mchezaji huru klabuni hapo kupisha usajili wa damu changa ambao utakuja kurudisha zama za mafanikio klabuni hapo.

Katika miaka yake mitano klabuni hapo Kennedy hawajawahi kuwa beki wa kutumainiwa ambapo mara nyingi alitumika kama chaguo la pili dhidi ya Pascal Wawa na Joash Onyango na msimu huu akisubiri kwa Henock Inonga na Che Fondoh Malone.

banner

Taarifa za ndani zinadai kuwa klabu za Pamba Jiji,Kagera Sugar na Mashujaa United zinaonyesha nia ya kumsajili beki huyo mkongwe hapa nchini akiwa na uzoefu wa kucheza michuano ya ndani na ya kimataifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited