Baada ya Awali kuifanyia umafia kwa Luis Miqquisone na Michael Sarpong klabu ya Simba sc imeifanyia umafia mwingine klabu ya Yanga baada ya kumsainisha beki wa pembeni wa Lipuli Fc David Kameta maarufu kama Duchu.
Awali Yanga iliripotiwa kumhitaji beki huyo na tayari ilianza mchakato wa kumsaninisha baada ya kocha Luc Eymael kumuhitaji lakini Simba imeingilia kati na kumsainisha beki huyo ikiwa na mapendekezo ya kocha Selemani Matola.
Taarifa zinadai Simba sc na Lipuli zimekubaliana na tayari mchezaji huyo amesaini mkataba wa awali wa miaka 3 na atatangazwa muda wa usajili ukifika.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.