Home Makala Simba sc Yamkataa Morrison

Simba sc Yamkataa Morrison

by Sports Leo
0 comments

Mabosi wa klabu ya Simba sc wamekubaliana kuachana na staa Benard Morrison mwishoni mwa msimu huu huku Nidhamu ikiwa ni kigezo kikubwa walichozingatia katika kufikia shauri hilo.

Mabosi hao walifikia maamuzi hayo kutokana na matukio kadhaa ya mshambuliaji huyo licha ya kuwa na nyakati nzuri za kuibeba timu hiyo tangu imsajili kutokea Yanga sc misimu miwili iliyopita.

Inaelezwa kocha Pablo Franco hapendezwi na wingi wa matukio ya nje ya uwanja ya staa huyo hasa kutokana na kuathiri mwenendo wa timu kwa ujumla huku klabu hiyo ikijipanga kusajili wachezaji wa maana ili kuwasaidia katika michuano ya kimataifa.

banner

Hata hivyo tayari inasemekana baadhi ya viongozi wa klabu ya Yanga sc wameanza mazungumzo na staa huyo ili kumrejesha klabuni hapo baada ya kuondoka misimu miwili iliyopita.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited