Home Makala Simba Sc Yatua Arusha Bila Camara,Che Malone

Simba Sc Yatua Arusha Bila Camara,Che Malone

by Sports Leo
0 comments

Msafara wa mastaa wa klabu ya Simba Sc umewasili salama katika mkoa wa Arusha mapema leo kulekea mchezo wa kesho wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Coastal Union.

Mchezo huo unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua utachezwa majira ya saa kumi jioni katika uwanja huo huku timu zote mbili zikiwa zimejipanga kuibuka na ushindi.

Katika msafara uliowasili mapema asubuhi ya leo wachezaji Moussa Camara na beki Che Malone Fondoh hawakuonekana katika msafara huo na kuendelea kuzua hofu pengine wanaweza kuukosa mchezo huo.

banner

Wachezaji hao hawakuwepo mazoezini katika siku ya alhamis jioni katika uwanja wa Mo Arena Bunju jijini Dar es Salaam ambapo waliumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc uliomalizika kwa sare ya 2-2.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited