Home Makala Staa Simba Sc Apata Dili Nono Hispania

Staa Simba Sc Apata Dili Nono Hispania

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba Sc Jean Charles Ahoua amepata ofa nono kutoka klabu ya Armelia Fc inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Hispania.

Mabosi wa klabu hiyo baada ya kuona video za michezo mbalimbali ya klabu ya Simba Sc anayoichezea mchezaji huyo wameridhika na uwezo wake na tayari wamefungua mazungumzo na menejimenti inayomsimamia mchezaji huyo.

Hata hivyo menejimenti hiyo imesema kuwa haiko tayari kwa sasa kujadili dili hilo mpaka mwishoni mwa msimu huu 2024-2025.

banner

“Tayari klabu hiyo imevutiwa na uwezo wa mchezaji huyo na wapo tayari kuanza mazungumzo ya kumsajili lakini sisi mpaka sasa hatuko tayari mpaka msimu uishe ndo tutaanza kuangalia ofa”,Alisema mmoja ya mabosi wa menejimenti ya mchezaji huyo

Ahoua amekua na msimu mzuri klabuni hapo akifunga mabao 15 mpaka sasa na akisaidia upatikanaji wa mabao saba mpaka sasa katika ligi kuu ya Nbc pekee.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited