Home Makala Stars Yapoteza Kwa Morocco

Stars Yapoteza Kwa Morocco

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Wanaume ya Tanzania (Taifa Stars) imepoteza mchezo wa kuwania kufuzu kombe la dunia mwaka 2026 dhidi ya Morocco baada ya kukubali kufungwa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika nchini humo.

Stars pamoja na kujitahidi kupambana lakini ilizidiwa uwezo na wenyeji ambapo mpaka kipindi cha kwanza matokeo yalisalia 0-0 licha ya kocha Hemed Morocco kumuanzisha kipa mgeni Yakub Selemani Ali wa Jkt Tanzania.

banner

Mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Manispaa nchini humo ulishuhudia Nayef Arguerd akifunga bao la kwanza dakika ya 51 kisha Brahim Diaz alifunga kwa penati dakika ya 58.

Sasa Morocco ni rasmi wamefuzu kushiriki kombe la dunia mwaka 2026 katika nchi za Mexico,Canada na Marekani baada ya kukusanya alama 15 kileleni mwa kundi E ikishinda michezo yote mitano huku Tanzania ikiwa nafasi ya tatu na alama sita sawa na Niger walionafasi ya pili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited