Home Makala Straika Awekewa Ngumu Kutua Simba sc

Straika Awekewa Ngumu Kutua Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Vipers Fc ya nchini Uganda bado imemweka ugumu mshambuliaji wake Cezar Manzoki kujiunga na klabu hiyo baada ya kukataa kiasi cha pesa ili kumuachia straika kujiunga na klabu ya Simba sc.

Awali klabu hiyo ilihitaji kiasi cha pesa ili kuvunja mkataba wa mchezaji huyo aliyetwaa tuzo tano za ligi kuu nchini humo katika msimu uliosha mwaka huu ambapo sasa klabu hiyo imebadili mawazo ikihitaji asalie klabuni hapo mpaka mkataba wake utakapoisha mwezi oktoba mwaka huu.

Vipers wanahitaji kiasi cha dola za kimarekani laki mbili ili kuvunja mkataba huo uliosalia miezi mitatu licha ya mchezaji huyo kuhitaji kuondoka akiwa tayari kununua hata sehemu ya mkataba wake uliosalia ili ajiunge na Simba sc.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited