Home Soka Straika Simba Sc Atua Zesco United

Straika Simba Sc Atua Zesco United

by Sports Leo
0 comments

Aliyekua mshambuliaji wa klabu ya Simba Sc Fredy Michael Koublan amesajili na klabu ya Zesco United inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Zambia kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Mshambuliaji huyo ambaye aliichezea Simba sc kwa miezi sita pekee alisajili kutokea klabu ya Green Eagle Fc ya nchini Zambia ambapo baada ya kushindwa kuonyesha kiwango alivunjiwa mkataba na nafasi yake kuzibwa na Lionel Ateba.

Awali mshambuliaji huyo ilikua ajiunge na Mc Algers ya nchini Algeria lakini kigezo cha kutokua na nafasi katika timu ya Taifa ya Ivory coast kuliharibu dili hilo na hatimaye alirejea nchini na kisha kufanya mazoezi binafsi akiungana na mastaa mbalimbali wa kigeni nchini.

banner

Klabu hiyo imethibitisha taarifa za kumsajili staa huyo kupitia mitandao yake ya kijamii ambapo ataanza rasmi kutumika baada ya dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited