Kocha mkuu wa Simba Sc,Sven Vandenbroeck amekanusha taarifa zilizoenea mtandaoni kuhusu nyota wake namba moja Meddie Kagere kuwa walipigana.
Sven amesema kuwa taarifa hizo si za kweli na hawezi kutumia nguvu kulizungumzia hilo kwakuwa halina maana kwani hajui wapi lilipotokea hadi kuzuka mitandaoni.
“Ninaloweza kusema ni kuwa sina tatizo na Meddie Kagere”alisema Sven baada yakutotaka mahojiano marefu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Sven ameshaanza kazi ya kukinoa kikosi chake cha Simba kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa ligi kuu bara msimu wa 2020/2021 unaotarajiwa kuchezwa Septemba 6, Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya dhidi ya Ihefu.