Home Soka Tabora United Yakana Chikola Kujiunga na Kmc

Tabora United Yakana Chikola Kujiunga na Kmc

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Tabora United imekana kuhusu kuachana na mshambuliaji wake Offen Chikola ambaye ameripotiwa kujiunga na Klabu ya Kmc Fc yenye makazi yake jijini Dar es Salaam.

Taarifa za awali zilieleza kuwa klabu ya Kmc imekamilisha usajili wa Chikola kutoka Tabora United kuchukua nafasi ya kiungo mshambuliaji wake Ibrahim Elias ambaye hayupo katika kambi ya timu hiyo mpaka sasa.

banner

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa Klabu hiyo umesema kuwa mchezaji huyo ana mkataba na klabu hiyo mpaka mwisho wa msimu huu hivyo hajaondoka klabuni hapo.

Msimu huu Chikola amekua msaada mkubwa klabuni hapo akiungana na Heritier Makambo na Yacouba Sogne kuunda safu hatari ya ushambuliaji iliyoifikisha timu hiyo katika nafasi ya tano ya msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited