Site icon Sports Leo

Uchebe Atambulishwa Rasmi Leopards

Timu ya Afc Leopard ya nchini Kenya imemtangaza rasmi kocha Patrick Aussems raia wa Ubeligiji kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.

Aussems ambaye anafahamika kwa jina la utani kama Uchebe amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Anthony Kimani ambaye ni mchezaji wa zamani nchini Kenya aliyejiuzuru na kumuachia nafasi kocha huyo mwenye miaka 55.

Raia wengi nchini Kenya wamepongeza usajili wa kocha huyo kutokana na kuwa na rekodi nzuri katika klabu kadhaa ambazo amepitia ikiwemo Simba sc pamoja na Al Hilal ya Sudan.

Exit mobile version